Social Icons

Friday, November 22, 2013

KAMATI KUU YA CHADEMA YAWAVUA UONGOZI ZITTO KABWE, DR KITILA MKUMBO NA SAMSONI MWIGAMBA



Kamati kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema imewavua Uongozi Viongozi wake watatu baada ya Kugundua waraka wa Siri uliowahusisha na mpango wa kukipasua Chama vipande vipande. Viongozi waliovuliwa Uongozi ni Zitto Kabwe ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Dr Kitila Mkumbo na Samsoni Mwigamba aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini. Hatua hiyo ilichukuliwa katika kikao cha kamati kuu kulichokuwa kimefanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.

Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari Mh Tundu Lissu amesema katika Waraka huo kulikuwa na mtu anayejukana kama MM ambaye ni Naibu Katibu mkuu Zitto Kabwe, M1 ni Dr Kitila Mkumbo, M3 ni Samsoni Mwigamba na M2 hajajulikana ambaye ni mtumishi wa makao makuu ya Chadema. Mh Lissu amesema Dr Kitila Mkumbo alikana kabisa kumfahamu M2. Mh Tundu Lissu amesema Waraka huo uliojulikana kama Waraka wa Ushindi unavunja katiba ya Chama kwa sababu umepandikiza chuki za kidini, majungu na kukashifu viongozi wa Chama kinyume na katiba ya CHADEMA. Mh Tundu Lissu amesema tuhuma zote zilizoko katika waraka huo hazijawahi kuwasilishwa kwenye kikao chochote halali cha chama kinyume na matakwa na masharti ya katiba yetu. Mh Tundu Lissu 
Amesema Kamati Kuu imeamua kuwavua nyadhifa zao zote watu wote waliotajwa katika waraka huo ambao ni Zitto Kabwe, Dr. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba.
Pia kamati kuu imeunda kamati ya kuchunguza na kufuatilia mhusika mwingine M2 ambaye anadaiwa ni Mtumishi wa Makao Makuu ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi yake
Kamati Kuu imeagiza wahusika wote waandikiwe barua za kujieleza ni kwanini wasivuliwe uanachama kwa makosa hayo makubwa waliyofanya.

Pia Kamati Kuu imeagiza mchakato wa kumvua Zitto nafasi yake ya Unaibu wa Kambi ya Upinzani Bungeni.
Lissu amesema Naibu Katibu Mkuu Zitto Kabwe na Dr. Kitila Mkumbo waliomba kujiuzulu nyadhifa zao zote baada ya waraka wao kukamatwa lakini Kamati Kuu iliwakatilia baada ya kuona kuwa kukubaliana na maombi yao hayo ilikuwa ni kama kuwaacha wajiuzulu kwa heshima ambayo hawaistahili hata kidogo.
Wakati huo huo kamati kuu imemteua Mh Tundu Lissu kuwa Mwanasheria mkuu wa Chama.

KAMATI KUU YA CHADEMA YAWAVUA UONGOZI ZITTO KABWE, DR KITILA MKUMBO NA SAMSONI MWIGAMBA



Kamati kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema imewavua Uongozi Viongozi wake watatu baada ya Kugundua waraka wa Siri uliowahusisha na mpango wa kukipasua Chama vipande vipande. Viongozi waliovuliwa Uongozi ni Zitto Kabwe ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Dr Kitila Mkumbo na Samsoni Mwigamba aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini. Hatua hiyo ilichukuliwa katika kikao cha kamati kuu kulichokuwa kimefanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.

Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari Mh Tundu Lissu amesema katika Waraka huo kulikuwa na mtu anayejukana kama MM ambaye ni Naibu Katibu mkuu Zitto Kabwe, M1 ni Dr Kitila Mkumbo, M3 ni Samsoni Mwigamba na M2 hajajulikana ambaye ni mtumishi wa makao makuu ya Chadema. Mh Lissu amesema Dr Kitila Mkumbo alikana kabisa kumfahamu M2. Mh Tundu Lissu amesema Waraka huo uliojulikana kama Waraka wa Ushindi unavunja katiba ya Chama kwa sababu umepandikiza chuki za kidini, majungu na kukashifu viongozi wa Chama kinyume na katiba ya CHADEMA. Mh Tundu Lissu amesema tuhuma zote zilizoko katika waraka huo hazijawahi kuwasilishwa kwenye kikao chochote halali cha chama kinyume na matakwa na masharti ya katiba yetu. Mh Tundu Lissu 
Amesema Kamati Kuu imeamua kuwavua nyadhifa zao zote watu wote waliotajwa katika waraka huo ambao ni Zitto Kabwe, Dr. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba.
Pia kamati kuu imeunda kamati ya kuchunguza na kufuatilia mhusika mwingine M2 ambaye anadaiwa ni Mtumishi wa Makao Makuu ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi yake
Kamati Kuu imeagiza wahusika wote waandikiwe barua za kujieleza ni kwanini wasivuliwe uanachama kwa makosa hayo makubwa waliyofanya.

Pia Kamati Kuu imeagiza mchakato wa kumvua Zitto nafasi yake ya Unaibu wa Kambi ya Upinzani Bungeni.
Lissu amesema Naibu Katibu Mkuu Zitto Kabwe na Dr. Kitila Mkumbo waliomba kujiuzulu nyadhifa zao zote baada ya waraka wao kukamatwa lakini Kamati Kuu iliwakatilia baada ya kuona kuwa kukubaliana na maombi yao hayo ilikuwa ni kama kuwaacha wajiuzulu kwa heshima ambayo hawaistahili hata kidogo.
Wakati huo huo kamati kuu imemteua Mh Tundu Lissu kuwa Mwanasheria mkuu wa Chama.

Wednesday, January 2, 2013

NMB MAKETE YAMWAGA ZAWADI KWA WAGONJWA




Katika kusherekea sikuu ya mwakampya benki ya NMb tawi la Makete  ilitembea katika hospitali ya wilaya ya Makete na kuwaliwaza wagonjwa pamoja na kuwapa zawadi za mwaka mpya .
 
Meneja wa benki hiyo bwana Anyambilile Ambingile alisema hatua hiyo imekuja baada ya kuona niviziri wakaenda kuwaona wagonjwa ambao wapo katika hospitali hiyo ili kuwapa moyo wangonjwa pamoja na kuwapa zawadi za mwaka mpya jambo ambalo litawafanya waongeze matumaini kuweza kupona na baadaye kiruhusiwa kutoka na wao kama taasisi kuwapa faraja 
 
Adha Ambingile aliyaomba mashirika taasisi  za dini pamoja serikali kuiga mfano huo kwa kuwatembelea mara kwa mara watu kama hao kwani kwa kufanya hivyo kunaleta mahusiano mazuri kati ya jamii na taasisi “tunaomba jamii ielewe kuwa suala la kuwasaidi watu katika jamii ni la kila mtu aliyenacho ndo maana nasema mashika yaige mfano huu ilikujijengea mazingira mazuri na ushikiano mzura baina ya taasisi na jamii kwani kwa kufanya hivyo kutasadia jamii iwe na mtazamo mzuri na kwa taasisi hizo”alisema Ambingile
 
Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa wilaya Michael Guraka alipongeza kitendo hicho na kuwapongeza benki hiyo kwa kuwakumbuka wagonjwa hao ambao wamekuwa wakikosa furaha hasa katika msimu huu wa sikuu kwani huwa wanakosa liwazo kwaupande wake Rehema Mahenge ambaye alilazwa katika wodi ya wazazi alishukuru kwa uongozi mzima wa benki hiyo kwa kuwakumbuka wagonjwa na kuwaomba kundlea kufanya hayo zaidi katika siku za usoni na wasishi hapo

Monday, December 17, 2012

MBUNGE ATOA MILIONI MBILI KUFIKISHA UMEME KATIKA KIJIJI CHA IVALALILA



Naibu waziri wa maji na mbunge wa jimbo la Makete dk Binilithi Satano Mahenge akizingumza na wana nchi wa jimbo wananchi wilayani Makete hivi karibuni (picha na riziki mgaya)

Na Riziki Mgaya


Naibu waziri wa maji na mbuge wa jimbo la Makete DK Binilithi Mahenge ameahidi  kuchangia shilingi milioni mbili katika mradi wa umeme katika kijiji cha Ivalalila wilayani Makete mkoani Njombe.

Ahadi hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki hii mbele ya wananchi wa Ivalalila akitoa ahadi hiyo  Dk Mahenge alisema  jitihada za wananchi kujitoa na kuanzisha mradi huo wa umeme utokanao na maporomoko ya maji yaliyoko katika  kijiji hicho ni wakuungwa mkono na kila mpenda maendeleo.
 
Pia Mahenge aliwataka wananchi hao kutokata tamaa na maendeleo ya kijiji hicho na kuahidi kuendelea kukisaidia kijiji hicho   kwa kushirikiana  na halimashauri ya wilaya 
“nitawaunga mkono kwakushirikiana na halmashauri ya wilaya kwa kupitia mfuko wa jimbo ili kuwaunga mkono kwa jitihada za maendeleo nimefurahishwa sana na uwajibikaji wenu hii inatia moyo pia natoa rai yangu kwa wananchi wa sehemu nyingine waige mfano huu ili kujikwamua na umasikini” alisema Dk Mahenge.
 
 Awali Dk mahenge alifanya ziara yake katika kijiji cha Ndulamo kilichopo wilayani hapa  na kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho ambapo walitoa kero zao   mbele ya naibu wa maji ambaye pia ni mbuge wa jimbo hilo huku kero ya maji ikiwagusa sana  wananchi wakijiji hicho na wakalazimika kumueleza Dk Mahenge kilio cha maji  kilichopo kijijini hapo kuwa imekuwa ni moja kati ya vitu vinavyo changia kushuka kwa maendeleo kijijini hapo 
“tunateseka na adha ya maji tunaomba kama mbuge wetu ambaye unasikiliza vilio vya wanachi wako na kwa kuwa ni naibu waziri wa maji tusaidie”walisema wanakijiji hao.
 

Tuesday, December 11, 2012

NYUMBA YA MTUMISHI WA ZAHANATI KUGHARIMU MILIONI 36 MAKETE




Na Eddwin Moshi

Zaidi ya shilingi milioni 36 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa zahanati ya kijiji cha Ivilikinge kilichopo kata ya Isapulano wilayani Makete
Akizungumzia suala hilo ofisini kwake Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Mendrad Sanga amesema kwamba ujenzi huo ulianza mwezi Mei mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Februari mwakani
Amesema kwa sasa zahanati hiyo kwa sasa inawahudumu wawili ambapo mmoja kati yao anaishi kwenye nyumba ya kupanga
Katika ujenzi huo serikali imechangia kiasi cha silingi milioni 6 huku milioni 30 ni nguvu za wananchi wa kijiji hicho
Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo ameiomba serikali kuongeza kiasi cha fedha kwa ajili ya ujenzi huo kwa kuwa kiasi walichotoa ki kidogo kulingana na ujenzi huo

VITUO VYA KULELEA WATOTO YATIMA WILAYANI MAKETE VYATAKIWA KUBUNI MIRADI ENDELEVU YA KUENDESHA VITUO HIVYO

Watoto yatima wanaoishi katika kituo cha Fema Matamba

Baadhi ya vitu alivyovitoa mkuu wa wilaya

Mkuu wa wilaya ya Makete Mh.Josephine Matiro(katikati) akisikiliza wimbo unaoimbwa na watoto wanaoishi kwenye kituo hicho(hawapo pichani), kulia kwake ni Askofu wa dayosisi ya kusini magharibi Job Mbwilo na kushoto ni Msimamizi wa kituo Bi Ala Mbwilo


Kituo cha watoto yatima cha FEMA Matamba

Watoto hao wakimuaga mkuu wa wilaya


 
 Na Edwin Moshi
 
 Vituo vinavyolelea watoto yatima wilayani Makete vimetakiwa kubuni na kuanzisha miradi endelevu itakayosaidia vituo hivyo kuzidi kutoa huduma bila kutegemea wahisani mbalimbali
Imeonekana kwamba kwa kufanya hivyo kutasaidia vituo hivyo kuendelea kuwepo hata kama wafadhili hao watasitisha ufadhili katika vituo hivyo, miradi waliyobuni na kuitekeleza itasaidia kuendesha vituo hivyo
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro wakati alipotembelea kituo cha watoto yatima cha Fema Matamba kwa lengo la kutoa msaada kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho
Amesema huu sio muda wa kubweteka na kuwategemea wafadhili pekee badala yake ni kuangalia mbele zaidi kwa kuanzisha miradi mbalimbali kama kilimo ambvyo itasaidia kuleta kipato cha vituo hivyo hasa ukizingatia hivi sasa wahisani wengi wanaanza kujitoa kufadhili masuala mbalimbali
“Sijui kwa nini sisi waafrika tunabweteka sana tunapenda sana misaada na kulalamika kazi hakuna wakati fursa tunazichezea wenyewe tu, sasa sijui tunataka nini, tuamke tutumie fursa tulizo nazo sasa” alisema
Hata hivyo mkuu huyo amepongeza uongozi wa kituo hicho kwa kuwa na moyo wa kusaidia kulea watoto hao yatima ambao mara nyingi jamii imewasahau, na kusema kuwa malipo ya kazi yao yatatolewa na mwenyezi MUNGU
Awali akitoa maelezo kuhusu kituo kwa Mh. Mkuuwa wilaya, msimamizi wa kituo hicho cha Fema Matamba Bi.Ala Mbwilo amesema kituo hicho kinategemea msaada wa wafadhili waliopo nje ya nchi ambao hutoa sh. Milioni 2 kila mwaka fedha ambazo bado hazitoshi kuendesha kituo hicho
Pamoja na hayo amesema ukosefua wa maji nalo ni tatizo lililopo eneo la Matamba ambalo huwalazimu kwenda mtoni kuchota maji ama kwenye bomba za vijiji jirani kwa ajili ya mahitaji ya kituo hicho
“Unajua mkuu watu huwa tunabweteka sana, hatutaki kulima wala kujishughulisha lakini tunapenda misaada tu, sasa misaada ikiisha tunakosa cha kufanya, tunabaki njia panda” alisema Bi. Mbwilo
Naye Askofu wa dayosisi ya kusini magharibi ambayo inamiliki kituo hicho Job Mbwilo ameshukuru kwa ujio huo wa mkuu wa wilaya huku akisema yeye ni kiongozi wa kwanza kufanya ziara ya kutembelea kituo hicho na kutoa msaada kwa watoto yatima wanaoishi hapo
Amesema wazo alilolitoa la kituo hicho kuwa na miradi endelevu watalifanyia kazi haraka iwezekanavyo kama namna ya kuboresha kituo hicho kwa kuwa jukumu la kuhakikisha watoto yatima popote duniani ni la jamii nzima, hivyo jamii nayo inapaswa kushirikiana kwa pamoja kuwalea watoto hao

Monday, December 3, 2012

MKUU WA WILAYA YA MAKETE AFANYA ZIARA KWENYE MFEREJI WA UMWAGILIAJI KATA YA LUWUMBU



Chanzo cha mfereji huo


Sehemu ya mfereji huo
Matumizi ya mfereji wa umwagiliaji kwenye mashamba ya wakulima katika kata ya Luwumbu wilayani Makete huenda yakaanza mwishoni mwa mwezi huu kutokana na ujenzi wake kuwa katika hatua za mwisho
Hayo yamesemwa na mkandarasi anayetengeneza mfereji huo wakati akimweleza mkuu wa wilaya ya Makete mh. Josephine Matiro alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa mfereji huo
Amesema mfereji huo ambao unatakiwa ukamilike ndani ya kipindi cha miezi sita ambapo ni Februari Mwakani, lakini amesema kutokana na hatua ambayo wamefikia sasa ni zaidi ya asilimia 85 na hatua zilizobakia ni chache hivyo ana uhakika wa kukamilisha kazi hiyo kabla ya Februari
Mfereji huo ambao unatarajiwa kuwa mkombozi kwa wakazi wa kata hiyo, umejengwa wakati muafaka ambapo mkuu huyo wa wilaya amempongeza mkandarasi huyo ambapo pamoja na mambo mengine amemsisitiza kuhakikisha anaujenga kww kiwango kinachokubalika na serikali, kwa kuwa kumaliza mradi kabla ya wakati uliopangwa mara nyingine ni jambo zuri ila kazi iwe ya kiwango stahili
“Unasikia ndugu mkandarasi, hongera kwa kazi nzuri na hatua uliyofikia lakini ndugu yangu hakikisha hii kazi inakuwa na viwango vinavyotakiwa kwa maana watakapokuja wakaguzi hapa kuikagua ikawa chini ya kiwango sijui utaiambia nini serikali, lakini ukimaliza mapema na ikawa ya kiwango kinachotakiwa kwa kweli ni jambo la heri” alisema Matiro
Wilaya ya Makete ni miongoni mwa wilaya chache hapa nchini zanye vyanzo vingi vya maji ambapo serikali imeanza mchakato wa kuvitumia vyanzo hivyo hivyo kwa uboreshaji wa shughuli za kilimo cha umwagiliaji ambapo imeanza utaratibu wa kutengeneza mifereji ya umwagiliaji

Saturday, November 24, 2012

PIKI PIKI ZA WAGONJWA ZAENDELEA KUOZA JK HAJUI HILO?

PIKI PIKI HIZI ZIPO HOSPITALI YA WILAYA MAKETE HAZIFANYI KAZI

WANYAMA KUZINDUA DARAJA DESEMBA MOSI MWAKA HUU

Baada ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara na Daraja la luwumbu kata ya luwumbu wilaya ya makete iliyojengwa kwa msaada wa mfanya biashara maalufu jijini dar es salaam Bwana Wanyama na wananchi kuanza kulitumia uzinduzi wadaraja hilo unatarajiwa kufanyika tarehe mosi desemba mwaka huu

akizungumza na mtandao huu Mfanya biashara huyo amesema uzinduzi huo utafanyika siku ya juma mosi na wanatarajia kuwaaalika watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa kisiasa na wa serikali na wananchi wote wa kata yaluwumbu na maeneo jirani

akizungumzi uamuzi wake wa kujenga daraja hilo Bwana Wanyama amesema kijiji cha luwumbu ndiko aliko zaliwa na tangu utoto wake amekuwa akiona wazazi wake wakipata shida ya kuvuka katika daraja dogo la miti lililokuwepo katika mto huo hivyo ameamua kuonyesha mchango wake kwa jamii ya wana luwumbu

aidha amewataka wafanyabiashara wenzake na watu wenye mafanikio kusaidia kule walikotoka ili kuwapunguzia matatizo ndugu zao wa kipato cha chini na wale wasio na uwezo kama wao

hii itakuwa cni mara ya kwanza kwa mfanya biashara kuamua kusimamia ujenzi mkubwa kama huo ulio gharimu pesa nyingi kama huo kwani daraja hilo pamoja na barabara vimegharimu zaidi ya shilingi milioni sabini

Wednesday, November 14, 2012

UJENZI ZAHANATI YA IVALALILA WASUASUA



Na Hadija Sanga
Zaidi ya shilingi milioni 80 zimetumika hadi sasa katika ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Ivalalila wilayani Makete, ujenzi ambao bado unaendelea
Hayo yamesemwa na Afisa mtendaji wa kijiji cha Ivalalila Bw. Fidelis Sanga alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na ujenzi huo ambao ulianza tangu mwaka 2010 kwa nguvu za wananchi kwa kushirikiana na serikali
Amesema mpaka sasa ujenzi huo unaendelea vizuri na umefikia hatua ya upauaji wa jengo hilo huku akisisitiza kuwa mradi huo umepokelewa kwa mikono miwili na wananchi wa kijiji hicho na ndio maana ujenzi huo umefikia hatua nzuri
Bw. Sanga amezitaja baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo kwa sasa katika ujenzi huo kuwa ni pamoja na uhaba wa fedha za kuendelea na mradi huo pamoja na uchache wa wananchi wanaokuja kushiriki katika ujenzi huo
Aidha ametoa wito kwa serikali na wadau mbalimbali kujumuika pamoja kushiriki ujenzi wa zahanati hiyo kwa namna moja ama nyingine pamoja na wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye shughuli za ujenzi huo pale wanapohitajika kufanya hivyo
 
Habari Kwa msaada wa Eddymoblaze.blogspot.com

MAMLAKA YA MAJI MAKETE YA HIMIZA UTUNZAJI WA VYANZO VYA MAJI


 chanzo cha maji Ivalalila
Chanzo cha maji cha ivalalila kinacho hudumia wakazi wa Makete kinavyo onekana (Picha na Riziki Mgaya)

Mtumishi wa mamlaka ya maji akishiriki zoezi la upandaji miti pembezoni mwa chanzo hicho cha maji
Mamlaka ya maji makete imeanza mikakati ya kuboresha huduma hiyo ili kuondokana na shida ya upatikanaji wa maji kwa watumiaji wa huduma hiyo.
Akizungumza na mtandao huu meneja wa Maji Bwana Jornas Ndomba amesema kuwa tayari wameshanza  jitihada za kuongeza kingo za pembeni katika chanzo kikuu cha maji kilichopo katika kijiji cha Ivalalila kwa Ajili ya kuzuia kupotea kwa maji mengi katika chanzo hicho
 
 
Sambamba na hilo pia mamlaka ya maji imepanda miti aina ya miturunga kuzunguka eneo la chanzo hicho cha maji kwa ajili ya kusaidia uhifadhi wa kisima hicho kutoka na miti hiyo kuto tumia maji mengi.
  
Katika hatua nyingine bwana Ndomba amewaomba wakazi wa Ivalalila kukitunza chanzo hicho kwa kutoendeleza shughuli za kibinadamu katika chanzo hicho kwani kuna baadhi ya watu wamekuwa na tabia ya kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo ufugaji na upandaji wa miti bila kuzingatia sheria za uhifadhi wa vyanzo vya maji

Saturday, November 10, 2012

BARABARA YA LAMI MAKETE YA ENDELEA KUSOGEA

Ujenzi ukiendelea katika barabara ya Njombe Makete kwa kiwango cha lami (picha zote na Riziki Mgaya)
 
 
 
Wananchi waipongeza serikali kwa jitihada zake za kuhakikisha inaboresha miundombinunuya barabara wilayani Makete kwa kuongeza kilomita moja ya barabara ya lami baada ya kukamilika kipande cha awali cha Mang'oto Usungilo

Wakizungumza na mtandao huu Wananchi wa kijiji cha Usungilo kata ya Tandala wamesema kukamilika kwa kipande hicho kitasidia kwa kiwango kikubwa kupunguza adha waliyokuwa wakiipata watumiaji wa barabara hiyo hususani katika kipindi cha masika

wamesema eneo hilo lilikuwa likisumbua sana kutokana na udongo wake kuwa wamfinyanzi jambo lilokuwa likichangia kwa magari kukwama kutokana na kuchimbika sana

aidha wameiomba serikalio kumsimamia mkandarasi canopies international kufanya kazihiyo kwa wakati ili kuepusha adha inayoweza kujitokeza ya magari kukwama kipindi hichi ambacho mvua zimeanza kunyesha


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

Thursday, November 8, 2012

KUTOKUWEPO KWA CHOO KWA KWAMISHA UZINDUZI WA KITUO CHA WATOTO YATIMA


Kituo kilichojengwa kwa ajili ya kulelea watoto yatima kilichopo kijiji cha Maleutsi wilayani Makete kinakabiliwa na tatizo la kutokuwepo kwa vyoo.
Akizungumza na wanahabari kituoni hapo msimamizi wa kituo hicho Mchungaji Simoni Ilomo amesema kuwa tatizo la vyoo limekuwa likikwamisha uzinduzi wa kituo hicho kilichoanza  kujengwa takribani miaka miwili iliyopita chini udhamini wa kanisa la Batheli Morogoro.
Amesema ujenzi wa kituo hicho ulisimamiwa na Askofu Mkuu wa kanisa la Tanzania Assemblies of God  [T.A.G] na changamoto kubwa kwa sasa ni kutokuwepo kwa vyoo ambapo ujenzi wa vyoo vinavyohitajika inatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni kumi na tatu.
Katika hatua nyingine Mch. Ilomo ameongeza kuwa kituo hicho mara  baada ya kuzinduliwa kitaanza kupokea watoto waishio katika mazingira hatarishi na yatima bila kubagua ukabila wala dini na wanatarajiwa kujenga chuo cha ufundi kwa ajili ya watakaoshindwa kuendelea  na sekondari au kidato cha sita.
Hata hivyo amesema watoto watakaolelewa pamoja na kusomeshwa na kituo hicho ni wale walio chini ya umri ya miaka saba pia amewaomba wahisani pamoja na serikali kusaidia ili kituo kianze kutoa huduma kwa watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Wednesday, November 7, 2012

MISAADA YA WATOTO YATIMA LAZIMA IWANUFAISHE WATOTO WENYEWE


watoto yatima wakiwa na magodoro yao

Wafanyakazi wa shirika la ELCT Makete - Pamoja Tuwalee program

Mratibu wa pamoja tuwalee MCh. Ezekiel Sanga (katikati) akiwa na wafanyakazi wenzake


Mgeni rasmi Mh. Daniel Okoka akimgawia mtoto yatima viatu


Mh. Daniel Okoka akitoa hotuba yake
Serikali imewataka viongozi wa kijiji cha Lumage kata ya Iniho wilayani Makete kuhakikisha inafuatilia na kujua kama nyumba ni hitaji muhimu la watoto yatima waliopo kwenye kijiji hicho pamoja na walezi kutowanyang’anya misaada wanayopewa watoto hao na kuifanya yao
Hayo yamesemwa na Mgeni rasmi katika hafla ya kugawa magodoro tisa kwa watoto yatima waliopo kijijini hapo yaliyotolewa na kikundi cha kuweka na kukopa kijijini hapo ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh. Daniel Okoka
Mh. Okoka amesema wakati mwingine ni vigumu kuona mtoto yatima hana hata ndugu mmoja hivyo anakosa mahali pa kukaa, ila anachoamini ni kwamba watoto hao wana ndugu lakini wengi wao wanawatesa watoto hao
“Ndugu zangu mimi sidhani kama kuna mtoto hata mmoja ambaye hana ndugu, inawezekana yupo lakini sina uhakika, ndugu walioachiwa watoto hawa wanapaswa kuwatunza kwa upendo ili wasitoroke majumbani” alisema Okoka na kuongeza “ leo tumewapa magodoro haya, ni kwa ajili ya watoto yatima sasa walezi masije mkawanyang’anya watoto na mkayafanya ya kwenu kwa sababu hiyo ndiyo tabia ya watu wengi, mnamnyang’anya mtoto godoro yeye anaendelea kulala chini, watoto mkiona mmefanyiwa hivyo toa taarifa kwa uongozi wa kijiji haraka”
Akizungumzia ushirikiano uliofanywa na Mratibu wa program ya Pamoja Tuwalee wilayani hapa Mch. Ezekiel Sanga, mh Okoka amesema serikali inatambua msaada unaotolewa na mashirika ya dini kuleta maendeleo hivyo akaomba ushirikiano huo uendelee zaidi na zaidi
Pia amesema wazo la program hiyo kuanzisha vikundi vya SILK ni muhimu na lenye kuinua kipato cha wananchi wake huku akisema uongozi wa wilaya ya Makete upo kwenye mchakato wa kuanzisha Benki ya wananchi wa Makete ambayo itakuwa ikishirikiana na vikundi hivyo vya SILK kuinua uchumi wa wanamakete
“Nawahakikishieni sisi kama wilaya tumeshakutana na wanamakete waliopo Dar es Salaam ambao wanafanya kazi kwenye benki mbalimbali na hata kwenye nafasi zingine, wamekubali na wanalishughulikia na muda si mrefu benki hiyo itaanza” alisema Okoka
Katika kukiunga mkono kikundi hicho mgeni rasmi Mh. Okoka alikipa shilingi 50,000/= pamoja na ada ya kujiunga kama mwanachama wa kikundi hicho ya shilingi 50,000/=, viatu kwa watoto hao yatima pamoja na kuahidi kutoa shuka na blanketi kwa kila mtoto aliyepewa godoro
Akizungumza hatua hiyo mratibu wa Program ya Pamoja Tuwalee inayofanya shughuli hiyo kupitia shirika la ELCT Makete Mch. Ezekiel Sanga amesema jukumu la kuwalea watoto yatima ni la kila mmoja hivyo kila mmoja wetu anapaswa kuwasaidia kwa chochote kile ili kuwapa faraja kutokana na kupoteza wazazi wao
Katika kuliunga mkono hilo Mchungaji huyo alianzisha harambee Fulani ya fedha kwa ajili ya yatima katika kijiji hicho ambapo jumla ya fedha taslim tsh. 153,600/- zilichangwa kwa ajili ya watoto yatima wengine kununuliwa mahitaji mbalimbali

Saturday, November 3, 2012

MAFUNZO YA MGAMBO YA FUNGWA RASMI LEO



 Mgambo wenyewe
 Mshauri wa mgambo wilaya ya Makete Bw. Mfuse
Mkuu wawilaya ya makete Bi Josephin Matilo akifunga mafunzo hayo
 Mgambo akisoma risala kwa mgeni rasmi


 Mkuu wa wilaya akigawa vitambulisho kwa mgambo
 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro(wa pili kulia) akicheza muziki na mgambo hao

Vijana mia moja na ishirini na mbili wahitimu mafunzo ya mgambo katika kata za Iwawa na Tandala huku wengine sabini na nane wakishindwa kumaliza mafunzo hayo kutokana na sababu za ugonjwa na wengine wakikimbia mafunzo hayo

Akifunga mafunzo hayo mkuu wa wilaya ya Makete Bi Josephin Matiro amewapongeza wa hitimu hao kwa uvumilivu na kujituma kwao hadi hitimu mafunzo hayo yaliyodumu kwa miezi minne

Amesema mafunzo hayo yanalengo la kuisaidia jamii kulinda mali zao lakini pia yana wasaidia wahitimu mbinu mbali mbali za kupambana na uhalifu na kupata mbinu za  kujitegemea  kimaendeleo

Aidha Bi Josephin ameahidi kuanzisha kambi ya vijana itakayo jihusisha na kilimo cha kisasa kilimo kitakacho wasaidia kuondokana na umaskini unao wakabili watanzania wengi lakini pia mpango huo utasaidia kupunguza tatizo la ajira kwao

Amesema vijana wengi wamekuwa wakilalamikia swala la ukosefu wa ajira wakati kuna fursa nyingi za kuweza kuwasaidia kuji kwamua kimaisha moja wapo ikiwa ni kutumia ardi iliyopo kwa matumizi ya kilimo

Amewataka vijana hao kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wengine walio shindwa kuendelea na mafunzo hayo kwa kufanya mambo yasiyo kinyume na maadili na sheri za nchi huku wakichangamkia fursa mbalimbali zinazo jitokeza katika wilaya yao

Kwa upande wao wahitmu wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kupambana na uharifu kuzuia mianya ya Rushwa na vilevile wamefundishwa mbinu za kupambana na umaskini kutokana na mafunzo ya kujitegemea waliyopewa

Aidha wameiomba serikali kuongeza posho kwa wa kufunzi wanao jitolea kwani wamefanya kazi kubwa kwa mda miezi minne lakini malipo wanayopewa ni kidogo mno na kutaka wenzao walioshindwa kumaliza mafunzo hayo kwa uvivu wachukuliwe hatua za kisheria ili kuyafanya mafunzo hayo yaonekane ya maana

Kwa upande wake Diwani Wakata ya Tandala Mheshimiwa Agnatio Mtawa amesema kambi ya vijana itaundwa kuonyesha kuwea wanaunga mkono harakati za mkuu wa wilaya ya makete Bi Josephin Matiro za kuondoa umaskini hususani kwa vijana

Aidha amewapongeza wahitimu hao na kusema kuwa atashirikiana nao kwa kila jambo watakalo hitaji kutoka kwake ili kuhakikisha raia wanakuwa salam pamoja na malizao lakini pia ili kuondoa dhana ya kwamba vijana hao walikuwa wakipoteza muda katika mafunzo hayo.   

WAFANYA BIASHARA MAKETE WAAMUA KUONYESHA UWEZO WAO HALMASHAURI YA MAKTE HAINA FEDHA

Mafundi wakiendelea na ujenzi wa choo cha soko



Vyoo vilivyo jengwa na halmashauri vilivyo jaa

Kibanda cha kukusanyia mapato ya halmashauri kwa wanao kwenda kupata huduma ya choo
soko la vyakula linavyo onekana 
Wafanyabiashara wa soko la makete waendelea na ujenzi wa choo cha soko baada ya ongozi wa halmashauri ya wilaya ya makete kukataa kujenga choo hicho kilicho ndani ya eneo la halmashauri

Akizungumza na mtandao huu mwenyekiti wa soko bwana Hosia Mpandila amesema baada ya halmashauri kukataa kusaidia ujenzi huo kwa madai ya kutokuwa na fedha waliamua kuanza kuchangishana fedha za ujenzi huo ambapo kila mfanya biashara alichangia kiasi cha shilingi elfu kumi

Amesema kweasasa wamemaliza ujenzi wa shimo na wameanza ujenzi wa vyumba ambao unaendelea vizuri na kuwataka wafanya biashara ambao hawajakamilisha michango yao kuiwasilisha kwa wakati kwa viongozi wa kamati ya ujenzi wa choo hicho

Amesema awali choo kilikuwa kinajengwa na halmashauri ya wilaya ya makete lakini wameshangazwa na kitendo cha halmashauri kukataa kuwasaidia ujenzi huo huku wakitishiwa kuhamishiwa katika soko la ngiu kama hawata jenga choo hicho

Soko lamakete mjini lina wafanya biashara wapatao miambili na watu wanoingia kuhudumiwa hapo wanakadiliwa kuwa ni mianne kwa siku jambo ambalo ni hatari kwa afya zao kama pasipo kuwa na choo cha uhakika.