Mgambo wenyewe
Mshauri wa mgambo wilaya ya Makete Bw. Mfuse
![]() |
Mkuu wawilaya ya makete Bi Josephin Matilo akifunga mafunzo hayo |
Mgambo akisoma risala kwa mgeni rasmi
Mkuu wa wilaya akigawa vitambulisho kwa mgambo
Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro(wa pili kulia) akicheza muziki na mgambo hao
Akifunga mafunzo hayo mkuu wa
wilaya ya Makete Bi Josephin Matiro amewapongeza wa hitimu hao kwa uvumilivu na
kujituma kwao hadi hitimu mafunzo hayo yaliyodumu kwa miezi minne
Amesema mafunzo hayo
yanalengo la kuisaidia jamii kulinda mali zao lakini pia yana wasaidia
wahitimu mbinu mbali mbali za kupambana na uhalifu na kupata mbinu za kujitegemea
kimaendeleo
Aidha Bi Josephin ameahidi
kuanzisha kambi ya vijana itakayo jihusisha na kilimo cha kisasa kilimo
kitakacho wasaidia kuondokana na umaskini unao wakabili watanzania wengi lakini
pia mpango huo utasaidia kupunguza tatizo la ajira kwao
Amesema vijana wengi wamekuwa
wakilalamikia swala la ukosefu wa ajira wakati kuna fursa nyingi za kuweza
kuwasaidia kuji kwamua kimaisha moja wapo ikiwa ni kutumia ardi iliyopo kwa
matumizi ya kilimo
Amewataka vijana hao kuwa
mfano wa kuigwa kwa vijana wengine walio shindwa kuendelea na mafunzo hayo kwa
kufanya mambo yasiyo kinyume na maadili na sheri za nchi huku wakichangamkia
fursa mbalimbali zinazo jitokeza katika wilaya yao
Kwa upande wao wahitmu
wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kupambana na uharifu kuzuia mianya ya Rushwa
na vilevile wamefundishwa mbinu za kupambana na umaskini kutokana na mafunzo ya
kujitegemea waliyopewa
Aidha wameiomba serikali
kuongeza posho kwa wa kufunzi wanao jitolea kwani wamefanya kazi kubwa kwa mda
miezi minne lakini malipo wanayopewa ni kidogo mno na kutaka wenzao
walioshindwa kumaliza mafunzo hayo kwa uvivu wachukuliwe hatua za kisheria ili
kuyafanya mafunzo hayo yaonekane ya maana
Kwa upande wake Diwani Wakata
ya Tandala Mheshimiwa Agnatio Mtawa amesema kambi ya vijana itaundwa kuonyesha
kuwea wanaunga mkono harakati za mkuu wa wilaya ya makete Bi Josephin Matiro za
kuondoa umaskini hususani kwa vijana
Aidha amewapongeza wahitimu
hao na kusema kuwa atashirikiana nao kwa kila jambo watakalo hitaji kutoka
kwake ili kuhakikisha raia wanakuwa salam pamoja na malizao lakini pia ili
kuondoa dhana ya kwamba vijana hao walikuwa wakipoteza muda katika mafunzo
hayo.
No comments:
Post a Comment