Social Icons

Saturday, November 3, 2012

WAFANYA BIASHARA MAKETE WAAMUA KUONYESHA UWEZO WAO HALMASHAURI YA MAKTE HAINA FEDHA

Mafundi wakiendelea na ujenzi wa choo cha soko



Vyoo vilivyo jengwa na halmashauri vilivyo jaa

Kibanda cha kukusanyia mapato ya halmashauri kwa wanao kwenda kupata huduma ya choo
soko la vyakula linavyo onekana 
Wafanyabiashara wa soko la makete waendelea na ujenzi wa choo cha soko baada ya ongozi wa halmashauri ya wilaya ya makete kukataa kujenga choo hicho kilicho ndani ya eneo la halmashauri

Akizungumza na mtandao huu mwenyekiti wa soko bwana Hosia Mpandila amesema baada ya halmashauri kukataa kusaidia ujenzi huo kwa madai ya kutokuwa na fedha waliamua kuanza kuchangishana fedha za ujenzi huo ambapo kila mfanya biashara alichangia kiasi cha shilingi elfu kumi

Amesema kweasasa wamemaliza ujenzi wa shimo na wameanza ujenzi wa vyumba ambao unaendelea vizuri na kuwataka wafanya biashara ambao hawajakamilisha michango yao kuiwasilisha kwa wakati kwa viongozi wa kamati ya ujenzi wa choo hicho

Amesema awali choo kilikuwa kinajengwa na halmashauri ya wilaya ya makete lakini wameshangazwa na kitendo cha halmashauri kukataa kuwasaidia ujenzi huo huku wakitishiwa kuhamishiwa katika soko la ngiu kama hawata jenga choo hicho

Soko lamakete mjini lina wafanya biashara wapatao miambili na watu wanoingia kuhudumiwa hapo wanakadiliwa kuwa ni mianne kwa siku jambo ambalo ni hatari kwa afya zao kama pasipo kuwa na choo cha uhakika.

No comments:

Post a Comment