Social Icons

Tuesday, December 11, 2012

NYUMBA YA MTUMISHI WA ZAHANATI KUGHARIMU MILIONI 36 MAKETE




Na Eddwin Moshi

Zaidi ya shilingi milioni 36 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa zahanati ya kijiji cha Ivilikinge kilichopo kata ya Isapulano wilayani Makete
Akizungumzia suala hilo ofisini kwake Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Mendrad Sanga amesema kwamba ujenzi huo ulianza mwezi Mei mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Februari mwakani
Amesema kwa sasa zahanati hiyo kwa sasa inawahudumu wawili ambapo mmoja kati yao anaishi kwenye nyumba ya kupanga
Katika ujenzi huo serikali imechangia kiasi cha silingi milioni 6 huku milioni 30 ni nguvu za wananchi wa kijiji hicho
Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo ameiomba serikali kuongeza kiasi cha fedha kwa ajili ya ujenzi huo kwa kuwa kiasi walichotoa ki kidogo kulingana na ujenzi huo

No comments:

Post a Comment