Social Icons

Monday, December 3, 2012

MKUU WA WILAYA YA MAKETE AFANYA ZIARA KWENYE MFEREJI WA UMWAGILIAJI KATA YA LUWUMBU



Chanzo cha mfereji huo


Sehemu ya mfereji huo
Matumizi ya mfereji wa umwagiliaji kwenye mashamba ya wakulima katika kata ya Luwumbu wilayani Makete huenda yakaanza mwishoni mwa mwezi huu kutokana na ujenzi wake kuwa katika hatua za mwisho
Hayo yamesemwa na mkandarasi anayetengeneza mfereji huo wakati akimweleza mkuu wa wilaya ya Makete mh. Josephine Matiro alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa mfereji huo
Amesema mfereji huo ambao unatakiwa ukamilike ndani ya kipindi cha miezi sita ambapo ni Februari Mwakani, lakini amesema kutokana na hatua ambayo wamefikia sasa ni zaidi ya asilimia 85 na hatua zilizobakia ni chache hivyo ana uhakika wa kukamilisha kazi hiyo kabla ya Februari
Mfereji huo ambao unatarajiwa kuwa mkombozi kwa wakazi wa kata hiyo, umejengwa wakati muafaka ambapo mkuu huyo wa wilaya amempongeza mkandarasi huyo ambapo pamoja na mambo mengine amemsisitiza kuhakikisha anaujenga kww kiwango kinachokubalika na serikali, kwa kuwa kumaliza mradi kabla ya wakati uliopangwa mara nyingine ni jambo zuri ila kazi iwe ya kiwango stahili
“Unasikia ndugu mkandarasi, hongera kwa kazi nzuri na hatua uliyofikia lakini ndugu yangu hakikisha hii kazi inakuwa na viwango vinavyotakiwa kwa maana watakapokuja wakaguzi hapa kuikagua ikawa chini ya kiwango sijui utaiambia nini serikali, lakini ukimaliza mapema na ikawa ya kiwango kinachotakiwa kwa kweli ni jambo la heri” alisema Matiro
Wilaya ya Makete ni miongoni mwa wilaya chache hapa nchini zanye vyanzo vingi vya maji ambapo serikali imeanza mchakato wa kuvitumia vyanzo hivyo hivyo kwa uboreshaji wa shughuli za kilimo cha umwagiliaji ambapo imeanza utaratibu wa kutengeneza mifereji ya umwagiliaji

No comments:

Post a Comment