Social Icons

Saturday, November 10, 2012

BARABARA YA LAMI MAKETE YA ENDELEA KUSOGEA

Ujenzi ukiendelea katika barabara ya Njombe Makete kwa kiwango cha lami (picha zote na Riziki Mgaya)
 
 
 
Wananchi waipongeza serikali kwa jitihada zake za kuhakikisha inaboresha miundombinunuya barabara wilayani Makete kwa kuongeza kilomita moja ya barabara ya lami baada ya kukamilika kipande cha awali cha Mang'oto Usungilo

Wakizungumza na mtandao huu Wananchi wa kijiji cha Usungilo kata ya Tandala wamesema kukamilika kwa kipande hicho kitasidia kwa kiwango kikubwa kupunguza adha waliyokuwa wakiipata watumiaji wa barabara hiyo hususani katika kipindi cha masika

wamesema eneo hilo lilikuwa likisumbua sana kutokana na udongo wake kuwa wamfinyanzi jambo lilokuwa likichangia kwa magari kukwama kutokana na kuchimbika sana

aidha wameiomba serikalio kumsimamia mkandarasi canopies international kufanya kazihiyo kwa wakati ili kuepusha adha inayoweza kujitokeza ya magari kukwama kipindi hichi ambacho mvua zimeanza kunyesha


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

1 comment: