Watoto yatima wanaoishi katika kituo cha Fema Matamba
Baadhi ya vitu alivyovitoa mkuu wa wilaya
Mkuu
wa wilaya ya Makete Mh.Josephine Matiro(katikati) akisikiliza wimbo
unaoimbwa na watoto wanaoishi kwenye kituo hicho(hawapo pichani), kulia
kwake ni Askofu wa dayosisi ya kusini magharibi Job Mbwilo na kushoto ni
Msimamizi wa kituo Bi Ala Mbwilo
Kituo cha watoto yatima cha FEMA Matamba
Watoto hao wakimuaga mkuu wa wilaya
Na Edwin Moshi
Vituo vinavyolelea watoto yatima wilayani Makete
vimetakiwa kubuni na kuanzisha miradi endelevu itakayosaidia vituo hivyo kuzidi
kutoa huduma bila kutegemea wahisani mbalimbali
Imeonekana kwamba kwa kufanya hivyo kutasaidia vituo hivyo
kuendelea kuwepo hata kama wafadhili hao
watasitisha ufadhili katika vituo hivyo, miradi waliyobuni na kuitekeleza
itasaidia kuendesha vituo hivyo
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete Mh.
Josephine Matiro wakati alipotembelea kituo cha watoto yatima cha Fema Matamba
kwa lengo la kutoa msaada kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho
Amesema huu sio muda wa kubweteka na kuwategemea wafadhili
pekee badala yake ni kuangalia mbele zaidi kwa kuanzisha miradi mbalimbali kama kilimo ambvyo itasaidia kuleta kipato cha vituo
hivyo hasa ukizingatia hivi sasa wahisani wengi wanaanza kujitoa kufadhili
masuala mbalimbali
“Sijui kwa nini sisi waafrika tunabweteka sana
tunapenda sana
misaada na kulalamika kazi hakuna wakati fursa tunazichezea wenyewe tu, sasa
sijui tunataka nini, tuamke tutumie fursa tulizo nazo sasa” alisema
Hata hivyo mkuu huyo amepongeza uongozi wa kituo hicho kwa
kuwa na moyo wa kusaidia kulea watoto hao yatima ambao mara nyingi jamii
imewasahau, na kusema kuwa malipo ya kazi yao
yatatolewa na mwenyezi MUNGU
Awali akitoa maelezo kuhusu kituo kwa Mh. Mkuuwa wilaya,
msimamizi wa kituo hicho cha Fema Matamba Bi.Ala Mbwilo amesema kituo hicho
kinategemea msaada wa wafadhili waliopo nje ya nchi ambao hutoa sh. Milioni 2
kila mwaka fedha ambazo bado hazitoshi kuendesha kituo hicho
Pamoja na hayo amesema ukosefua wa maji nalo ni tatizo
lililopo eneo la Matamba ambalo huwalazimu kwenda mtoni kuchota maji ama kwenye
bomba za vijiji jirani kwa ajili ya mahitaji ya kituo hicho
“Unajua mkuu watu huwa tunabweteka sana, hatutaki kulima wala kujishughulisha
lakini tunapenda misaada tu, sasa misaada ikiisha tunakosa cha kufanya,
tunabaki njia panda” alisema Bi. Mbwilo
Naye Askofu wa dayosisi ya kusini magharibi ambayo
inamiliki kituo hicho Job Mbwilo ameshukuru kwa ujio huo wa mkuu wa wilaya huku
akisema yeye ni kiongozi wa kwanza kufanya ziara ya kutembelea kituo hicho na
kutoa msaada kwa watoto yatima wanaoishi hapo
Amesema wazo alilolitoa la kituo hicho kuwa na miradi
endelevu watalifanyia kazi haraka iwezekanavyo kama
namna ya kuboresha kituo hicho kwa kuwa jukumu la kuhakikisha watoto yatima
popote duniani ni la jamii nzima, hivyo jamii nayo inapaswa kushirikiana kwa pamoja
kuwalea watoto hao
Tunashukuru ila tunaomba misaada hiyo ifanye kazi kwa walengwa.
ReplyDelete