Social Icons

Wednesday, November 14, 2012

MAMLAKA YA MAJI MAKETE YA HIMIZA UTUNZAJI WA VYANZO VYA MAJI


 chanzo cha maji Ivalalila
Chanzo cha maji cha ivalalila kinacho hudumia wakazi wa Makete kinavyo onekana (Picha na Riziki Mgaya)

Mtumishi wa mamlaka ya maji akishiriki zoezi la upandaji miti pembezoni mwa chanzo hicho cha maji
Mamlaka ya maji makete imeanza mikakati ya kuboresha huduma hiyo ili kuondokana na shida ya upatikanaji wa maji kwa watumiaji wa huduma hiyo.
Akizungumza na mtandao huu meneja wa Maji Bwana Jornas Ndomba amesema kuwa tayari wameshanza  jitihada za kuongeza kingo za pembeni katika chanzo kikuu cha maji kilichopo katika kijiji cha Ivalalila kwa Ajili ya kuzuia kupotea kwa maji mengi katika chanzo hicho
 
 
Sambamba na hilo pia mamlaka ya maji imepanda miti aina ya miturunga kuzunguka eneo la chanzo hicho cha maji kwa ajili ya kusaidia uhifadhi wa kisima hicho kutoka na miti hiyo kuto tumia maji mengi.
  
Katika hatua nyingine bwana Ndomba amewaomba wakazi wa Ivalalila kukitunza chanzo hicho kwa kutoendeleza shughuli za kibinadamu katika chanzo hicho kwani kuna baadhi ya watu wamekuwa na tabia ya kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo ufugaji na upandaji wa miti bila kuzingatia sheria za uhifadhi wa vyanzo vya maji

No comments:

Post a Comment