Social Icons

Saturday, October 27, 2012

WALEMAVU NA WENYE VVU MAKETE WAPATIWA MBUZI WA KISASA



Jumla ya mbuzi 112 wamegawiwa kwa baadhi ya vikundi vya shirika la MASUPHA wilayani Makete kwa lengo la kuboresha lishe na kuinua uchumi wa vikundi hivyo
Akizungumza na mwanahabari wetu wakati wa ugawaji mbuzi hao, mkurugenzi wa shirikala MASUPHA Bi Aida Chengula amesema shirika hilo lilijadili kwa pamoja  na wanavikundi hao ambapo wao wenyewe walipendekeza kuwa wanahitaji mbuzi wa kisasa wa maziwa na ndiyo maana wamewapatia mbuzi hao
Bi Chengula amesema baadhi ya vikundi hivyo vinajumuisha walemavu na wenye virusi vya UKIMWI ambao mara nyingi husahaulika hivyo mbuzi hao watainua uchumi wao na kuongeza kuwa wamewapata mbuzi hao kwa ufadhili wa RFE
Naye afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka RFE Bw. Julius Mkandara amesema mbuzi hao wa kisasa ni faraja kwa wanavikundi hao na ni namna mojawapo ya kuheshimu mawazo yao
Amesema mbuzi hao watakapozaliana watapata maziwa ya kunywa na kuuza na mbuzi wa kuuza kama njia mojawapo ya kujipatia kipato pamoja na mbolea kwa ajili ya bustani za mbogamboga
Mmoja wa wanakikundi kutoka kata ya Isapulano aliyejitambulisha kwa jina la Monica Mahenge amesema mbuzi hao watamsaidia kuendesha familia ikiwemo kusomesha watoto
Shirika la MASUPHA limekuwa likisaidia kuvipa vikundi vyake mikopo yenye riba nafuu pamoja na misaada mbalimbali ikiwemo mifugo kama mbuzi kwa lengo la kuvikwamua kiuchumi

No comments:

Post a Comment