Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Daniel Okoka
Waheshimiwa
madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Makete wamefanya ukaguzi wa
barabara katika baadhi ya maeno katika kata ya Iwawa ambazo zilifanyiwa
ukarabati hivi karibuni
Akizungumza
na vyombo vya habari mara baada ya kumaliza ukaguzi huo wa kushtukiza
mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete mh. Daniel Okoka ambaye
aliongozana na madiwani wenzake amesema wameweza kukagua miundombinu ya
barabara kuelekea halmashauri ya Makete (Bomani), Tanesco na nyinginezo
za mitaa mbalimbali ya kata ya Iwawa
Mh.
Okoka amesema kuwa anawaomba wananchi kutokuharibu miundombinu kwa
kutupa takataka kwenye mifereji ya maji kandokando mwa barabara pamoja
na kwenye makalavati kwani vinaharibu barabara
Hata
hivyo Mh. Okoka amewaasa wananchi kutambua kuwa wao ni miongoni mwa
watu wanaotakiwa kutunza barabara hizo na pia ameongeza kuwa kabla ya
kuanza kwa matengenezo ya barabara wananchi watatakiwa kutoa maoni juu
ya ujenzi wa barabara
Ukaguzi
huo umefanywa kufuatia barabara hizo kujengwa chini ya kiwango, hali
iliyopelekewa kulaumiwa na wananchi, lakini Mh. Okoka hakutaka kuliweka hilo
wazi na badala yake amesema wameamua kufanya hivyo ili kuweza
kulijadili katika vikao vyao vya ndani na taarifa itatolewa baadaye
Amesema
badabara hizo zitatakiwa kufanyiwa marekebisho pamoja na kuzibuliwa kwa
mitaro iliyojiziba kwa vumbi jingi pamoja na kifusi kizuri kwenye
barabara hizo ili kuepuka vumbi lisilo na ulazima
No comments:
Post a Comment