Wananchi wilayani Makete wameshauriwa kutumia huduma za kibenki kutokana na elimu wanayoipata juu ya huduma hizo
Akizungumza
na wananchi wa kijiji cha Iwawa Meneja wa benki ya NMB tawi la Makete
Bw. Peter kinyosa amesema kuwa benki hiyo inatoa huduma ya kuweka na
kutoa fedha, mikopo pamoja na kufungua akaunti kwa wateja wapya
Amesema
matumizi ya huduma za kibenki hayana usumbufu hivyo ni wakati muafaka
kwa wananchi kuhifadhi fedha zao benki kwani ni sehemu salama na yenye
uhakika zaidi
Pia
meneja huyo ametoa wito kwa wateja wa benki yake kuhifadhi taarifa zao
za siri za kibenki ili kuepukana na wimbi la matapeli ambao wanaweza
kuwaibia fedha zao
Naye
afisa mikopo wa NMB Makete Bw. Rodrick Mollel amesema kuwa wananchi
wanatakiwa kutumia mikopo wanayoipata kufanyia shughuli za kimaendeleo
ili kuinua kipato chao pamoja na kunufaika na mikopo hiyo
No comments:
Post a Comment