Social Icons

Saturday, November 24, 2012

WANYAMA KUZINDUA DARAJA DESEMBA MOSI MWAKA HUU

Baada ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara na Daraja la luwumbu kata ya luwumbu wilaya ya makete iliyojengwa kwa msaada wa mfanya biashara maalufu jijini dar es salaam Bwana Wanyama na wananchi kuanza kulitumia uzinduzi wadaraja hilo unatarajiwa kufanyika tarehe mosi desemba mwaka huu

akizungumza na mtandao huu Mfanya biashara huyo amesema uzinduzi huo utafanyika siku ya juma mosi na wanatarajia kuwaaalika watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa kisiasa na wa serikali na wananchi wote wa kata yaluwumbu na maeneo jirani

akizungumzi uamuzi wake wa kujenga daraja hilo Bwana Wanyama amesema kijiji cha luwumbu ndiko aliko zaliwa na tangu utoto wake amekuwa akiona wazazi wake wakipata shida ya kuvuka katika daraja dogo la miti lililokuwepo katika mto huo hivyo ameamua kuonyesha mchango wake kwa jamii ya wana luwumbu

aidha amewataka wafanyabiashara wenzake na watu wenye mafanikio kusaidia kule walikotoka ili kuwapunguzia matatizo ndugu zao wa kipato cha chini na wale wasio na uwezo kama wao

hii itakuwa cni mara ya kwanza kwa mfanya biashara kuamua kusimamia ujenzi mkubwa kama huo ulio gharimu pesa nyingi kama huo kwani daraja hilo pamoja na barabara vimegharimu zaidi ya shilingi milioni sabini

No comments:

Post a Comment