Ikiwa
zimepita siku chache tangu wakala wa udhibiti wa nishati na maji EWURA
kuzuia shehena ya mafuta kusafirishwa nje ya nchi kutokana na uhaba wa
mafuta uliopo, bei za mafuta bado ni kubwa wilayani Makete.
Akizungumza
na mtandao huu muuzaji wa mafuta aina ya diesel na petroli Iwawa
mjini Bw. Alex Kyando amesema wamekuwa wakihahangaika kununua mafuta
hayo kulingana na uhaba unajitokeza.
Bw.Kyando
amesema bei za petrol na diesel zimepanda ikiwa petrol inauzwa kwa
shilingi 2500 kwa lita tofauti na hapo awali ambapo ilikuwa ikiuzwa
sh.2400 kwa lita na diesel inauzwa sh 2300 kwa lita moja toka awali.
Ameongeza
kuwa wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbaliikiwa ni pamoja na
uhaba wa mafuta,usumbufu kutoka kwa wateja na mabadiliko ya bei za mara
kwa mara za kushuka na kupanda kwa bidhaa hiyo
Hata
hivyo Bw.Kyando amewaomba wafanyabiashara wakubwa wa mafuta kupunguza
bei za mafuta ili kupungua kwa tatizo la uhaba wa bidhaa hiyo na
usumbufu unaojitokeza katika biashara hiyo.
No comments:
Post a Comment