Mkuu wa
shule ya msingi Ludihani iliyopo kijiji cha Ludihani wilayani Makete
amesema kuwa ujenzi wa nyumba ya walimu shuleni hapo bado unaendelea.
Akizungumza
na http://maketeyetu.blogspot.com/ ofisini kwake Mwalimu mkuu huyo Bw. Leo
Mahenge ameeleza kuwa ujenzi huo ulianza mwezi wa Machi 2012 mpaka sasa
unaendelea vizuri kutokana na nguvu za wananchi wa kijiji hicho.
Bw. Mahenge
ameongeza kuwa mpaka sasa ni nyumba moja tu ambayo tayari imekamilika
na anaishi mwalimu mkuu huyo na pia ujenzi wa nyumba hiyo umegharimu
milioni tatu na laki sita zilizotolewa na mpango wa maendeleo ya elimu
ya msingi [MMEM].
Hata hivyo
Bw. Mahenge amezitaja baadhi ya changamoto anazokabiliana nazo shuleni
hapo kuwa ni upungufu wa walimu pamoja na uchache wa nyumba za kuishi
walimu hao.
“Kweli
pamoja na changamoto kwa kweli ni upungufu wa waalimu natambua kuwa ni
tatizo la kitaifa lakini waalimu ni muhimu kwa shule yetu serikali
inatakiwa iliangalie hili kwani linakwenda sambamba na nyumba za
waalimu” alisema
No comments:
Post a Comment