Imeelezwa kuwa maandalizi ya ujenzi wa zahanati katika kijiji cha Ludihani Wilayani Makete bado yanaendelea.
Akizungumza na wanahabari
ofisini kwake Afisa Mtendaji wa kijiji cha Ludihani Bw.Dakta Jaska
Mahenge amesema kuwa eneo kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo tayari
limeandaliwa vikiwamo mchanga na mawe.
Bw.Mahenge amesema kuwa
wameshindwa kuanza ujenzi huo mara moja kutoka na ramani ya ujenzi wa
zahanati iliyotolewa na serikali kuwa kubwa ambapo amesema ujenzi wa
ramani ya sasa unakadiriwa kugharimu zaidi ya sh. Milioni 500 hivyo
kushindwa kumudu kiasi hicho kwa wakati kulingana na kipato kidogo
walicho nacho
Pia ameiomba serikali
itambue uwezo mdogo wa kifedha wa wananchi wake na kuwaomba wafadhili
mbalimbali wenye uwezo kujitokeza kutoa michango yao ili kufanikisha ujenzi huo.
Hata hivyo Bw. Mahenge
ameeleza changamoto ambazo wanakabiliana nazo kuwa ni pamoja na uhaba wa
mchanga wa kujengea kutokana na mchanga huo kutoka nje ya kijiji hicho
Bw.Mahenge anawaomba
wananchi kutoa michango kwa manufaa yao na pia kushiriki katika shughuli
za kimaendeleo kwani suala la ujenzi wa zahanati ni kwa ajili yao
kutokana na umbali wa zahanati wanalio nao kwa sasa.
No comments:
Post a Comment