Wananchi wa kijiji cha
Maleutsi wilayani Makete wametoa ushirikiano mzuri wa kifedha kwa ajili
ya ujenzi wa choo cha shule ya msingi Maleutsi kijijini hapo.
Akizungumza na maketeyetu.blogspot.com ofisini kwake Afisa mtendaji wa kijiji hicho
Bw.Michael Sanga amesema kwamba ujenzi wa choo hicho umeanza mwezi huu
ambapo shimo moja kubwa limeshakamilika na wanatarajia kuanza uchimbaji
wa shimo dogo shuleni hapo.
Bw.Sanga ameongeza kuwa wananchi wametoa michango yao ambapo kila mmoja amekuwa akichangia shilingi elfu kumi ikiwa shimo hilo
limegharimu kiasi cha shilingi milioni tatu ambapo mpaka kukamilika ili
kianze kutumiwa na wanafunzi choo hicho kitagharimu zaidi ya shilingi
milioni tisa.
“Ndugu mwandishi kimsingi mambo ya ujenzi yanakwenda vizuri ukizingatia hii
ni huduma muhimu kwa wanafunzi shuleni hapa, nashukuru wananchi wanatoa
michango yao kwa wakati na ndio maana ujenzi huu unafanikiwa” alisema Bw. Sanga
Katika hatua nyingine Bw.
Sanga amesema fedha zitakazomalizia ujenzi wa choo hicho wanatarajia
kuuza msitu wa shule hiyo ili kukamilisha sehemu iliyobaki kwa ajili ya
kuanza kutumika mwezi January 2013 na choo hicho kitatumia maji ambayo yataingizwa muda mfupi ujao kuanzia sasa.
“Uzuri ni kwamba shule hii
ina vitegauchumi vingi na kimojawapo ni msitu, hivyo tunatarajia kuuza
msitu wa shule na fedha zitakazopatikana tutazitumia kumallizia choo
hicho” alisema
No comments:
Post a Comment